Kauli


kechi kenyatta / expired giant

Kauli

By kechi kenyatta / expired giant

Mon 06 Mar, 2017 23:29:09 EAT
860 Views | 10 Comments | 96 Likes

#penzi  #uamizi  


Kauli

Anapocheza lelema
Ananifanya nileuke mwishowe naleleja
Umbo lake mviringo
Kiuno chake lembelembe
Hayo yote yanichanganya
Msimamo wangu huwa thabiti
Na tayari umegeuzwa kuwa legelege
Sio eti Mimi mlevi
Ila mwenzenu amerogwa na penzi.

Nina kanionya kumhusu,
Lakini naona nikikaidi.
Maana mtoto yule kaiva,
Rangi yake rajamu.


Rasilimali kwangu rasimu
Japo ramli ninayo
Ila si mwitaji rasuli
Ndipo ndoa yetu raufu

Heri niwe mtumwa
Na.nikubali utobwe
Na nihepe shadidi,
Maana upweke waeza niua,
Heri nifuate penyo.
Licha ya kuwa upeo.
Maana upatanisho ni ahera.



By kechi kenyatta / expired giant
Does this poem Deserve a thumbs up?
Yes

Download


Prev : Curved Destiny Next : Price Of Freedom



Sharing is Caring


Comments

  • Alice
    Heko
    368 wk ago
  • Chris
    Heko ndugu, si wengi wana uwezo wa kutungu ushairi kwa lugha ya Kiswahili. Mimi mmoja wao, mpenzi wa Kiswahili lakini naipa Kiingereza kipaumbele.
    368 wk ago
  • Isabella Nkirote
    Hata komenti ni ngori kudosi Kechi
    368 wk ago
  • Shiruha Victor
    Eeeee kweli mwenzetu karogwa na penzi. Swadakta!!!!!!!!
    368 wk ago
  • Rick Okinda
    ustadi wako ni wa kusisimua, una uwezo mkubwa was kuwa guru katika fani ya kuwa malenga, Nazi pevu mno bwana
    368 wk ago
  • Rapando Jnr
    Heko ndugu
    368 wk ago
  • Kelvin Achuka
    Swadakta!!!hongera
    368 wk ago
  • Quin Bernards
    The only word nmeelewa ni penzi.. Nice piece of art though sijaelewa half of it coz oswayo ni taabu
    368 wk ago
  • Nannah
    hongera kaka.......
    367 wk ago
  • Didy
    Swahili is hard but that chiq is praised lol.good job
    366 wk ago

Fields marked with * are required